1 : 1
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU . [1]
1 : 2
ٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Sifa njema zote ni za Mwenyeezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote; [2]
1 : 3
ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu; [3]
1 : 4
مَـٰلِكِ يَوْمِ ٱلدِّينِ
Mwenye kumiliki siku ya malipo. [4]
1 : 5
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ
Wewe tu tunakuabudu, na wewe tu tunakuomba msaada. [5]
1 : 6
ٱهْدِنَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
Tuongoe njia iliyonyooka. [6]
1 : 7
صِرَٰطَ ٱلَّذِينَ أَنْعَمْتَ عَلَيْهِمْ غَيْرِ ٱلْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ
Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea. [7]