37 : 1
وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. [1]
★
37 : 2
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا
Na kwa wenye kukataza mabaya. [2]
★
37 : 3
فَٱلتَّـٰلِيَـٰتِ ذِكْرًا
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. [3]
★
37 : 4
إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. [4]
★
37 : 5
رَّبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَـٰرِقِ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote. [5]
★
37 : 6
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota. [6]
★
37 : 7
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ مَّارِدٍ
Na kulinda na kila shet'ani a'si. [7]
★
37 : 8
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande. [8]
★
37 : 9
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. [9]
★
37 : 10
إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. [10]
★
37 : 11
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata. [11]
★
37 : 12
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. [12]
★
37 : 13
وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki. [13]
★
37 : 14
وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara. [14]
★
37 : 15
وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. [15]
★
37 : 16
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa? [16]
★
37 : 17
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Hata baba zetu wa zamani? [17]
★
37 : 18
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili. [18]
★
37 : 19
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona! [19]
★
37 : 20
وَقَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. [20]
★
37 : 21
هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha. [21]
★
37 : 22
۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu. [22]
★
37 : 23
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu! [23]
★
37 : 24
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: [24]
★
37 : 25
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Mna nini? Mbona hamsaidiani? [25]
★
37 : 26
بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Bali hii leo, watasalimu amri. [26]
★
37 : 27
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana. [27]
★
37 : 28
قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia. [28]
★
37 : 29
قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. [29]
★
37 : 30
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَـٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَـٰغِينَ
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu. [30]
★
37 : 31
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. [31]
★
37 : 32
فَأَغْوَيْنَـٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَـٰوِينَ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. [32]
★
37 : 33
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. [33]
★
37 : 34
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu. [34]
★
37 : 35
إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna. [35]
★
37 : 36
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? [36]
★
37 : 37
بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume. [37]
★
37 : 38
إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu. [38]
★
37 : 39
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya. [39]
★
37 : 40
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. [40]
★
37 : 41
أُو۟لَـٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Hao ndio watakao pata riziki maalumu, [41]
★
37 : 42
فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Matunda, nao watahishimiwa. [42]
★
37 : 43
فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani za neema. [43]
★
37 : 44
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ
Wako juu ya viti wamekabiliana. [44]
★
37 : 45
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem. [45]
★
37 : 46
بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّـٰرِبِينَ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao. [46]
★
37 : 47
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi. [47]
★
37 : 48
وَعِندَهُمْ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. [48]
★
37 : 49
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. [49]
★
37 : 50
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe. [50]
★
37 : 51
قَالَ قَآئِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌ
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki. [51]
★
37 : 52
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki. [52]
★
37 : 53
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa? [53]
★
37 : 54
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Atasema: Je! Nyie mnawaona? [54]
★
37 : 55
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu. [55]
★
37 : 56
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza. [56]
★
37 : 57
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. [57]
★
37 : 58
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Je! Sisi hatutakufa, [58]
★
37 : 59
إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa. [59]
★
37 : 60
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa. [60]
★
37 : 61
لِمِثْلِ هَـٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَـٰمِلُونَ
Kwa mfano wa haya nawatende watendao. [61]
★
37 : 62
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum? [62]
★
37 : 63
إِنَّا جَعَلْنَـٰهَا فِتْنَةً لِّلظَّـٰلِمِينَ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. [63]
★
37 : 64
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu. [64]
★
37 : 65
طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَـٰطِينِ
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. [65]
★
37 : 66
فَإِنَّهُمْ لَـَٔاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo. [66]
★
37 : 67
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. [67]
★
37 : 68
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. [68]
★
37 : 69
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea. [69]
★
37 : 70
فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَـٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. [70]
★
37 : 71
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. [71]
★
37 : 72
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. [72]
★
37 : 73
فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَـٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
Basi hebu angalia ulikuje mwisho wa walioonywa. [73]
★
37 : 74
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliokhitariwa. [74]
★
37 : 75
وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji. [75]
★
37 : 76
وَنَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa. [76]
★
37 : 77
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia. [77]
★
37 : 78
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. [78]
★
37 : 79
سَلَـٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِى ٱلْعَـٰلَمِينَ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote! [79]
★
37 : 80
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [80]
★
37 : 81
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. [81]
★
37 : 82
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Kisha tukawazamisha wale wengine. [82]
★
37 : 83
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake, [83]
★
37 : 84
إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima. [84]
★
37 : 85
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini? [85]
★
37 : 86
أَئِفْكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? [86]
★
37 : 87
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? [87]
★
37 : 88
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِى ٱلنُّجُومِ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota. [88]
★
37 : 89
فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! [89]
★
37 : 90
فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo. [90]
★
37 : 91
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli? [91]
★
37 : 92
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Mna nini hata hamsemi? [92]
★
37 : 93
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia. [93]
★
37 : 94
فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Basi wakamjia upesi upesi. [94]
★
37 : 95
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe [95]
★
37 : 96
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! [96]
★
37 : 97
قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَـٰنًا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo! [97]
★
37 : 98
فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًا فَجَعَلْنَـٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini. [98]
★
37 : 99
وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. [99]
★
37 : 100
رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. [100]
★
37 : 101
فَبَشَّرْنَـٰهُ بِغُلَـٰمٍ حَلِيمٍ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole. [101]
★
37 : 102
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَـٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri. [102]
★
37 : 103
فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. [103]
★
37 : 104
وَنَـٰدَيْنَـٰهُ أَن يَـٰٓإِبْرَٰهِيمُ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!. [104]
★
37 : 105
قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema. [105]
★
37 : 106
إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَـٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri. [106]
★
37 : 107
وَفَدَيْنَـٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. [107]
★
37 : 108
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. [108]
★
37 : 109
سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
Iwe salama kwa Ibrahim!. [109]
★
37 : 110
كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [110]
★
37 : 111
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. [111]
★
37 : 112
وَبَشَّرْنَـٰهُ بِإِسْحَـٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. [112]
★
37 : 113
وَبَـٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَـٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌ
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. [113]
★
37 : 114
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni. [114]
★
37 : 115
وَنَجَّيْنَـٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa. [115]
★
37 : 116
وَنَصَرْنَـٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda. [116]
★
37 : 117
وَءَاتَيْنَـٰهُمَا ٱلْكِتَـٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha. [117]
★
37 : 118
وَهَدَيْنَـٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. [118]
★
37 : 119
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. [119]
★
37 : 120
سَلَـٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!. [120]
★
37 : 121
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. [121]
★
37 : 122
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini. [122]
★
37 : 123
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. [123]
★
37 : 124
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?. [124]
★
37 : 125
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَـٰلِقِينَ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,. [125]
★
37 : 126
ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?. [126]
★
37 : 127
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;. [127]
★
37 : 128
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [128]
★
37 : 129
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. [129]
★
37 : 130
سَلَـٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
Iwe salama kwa Ilyas. [130]
★
37 : 131
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. [131]
★
37 : 132
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. [132]
★
37 : 133
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. [133]
★
37 : 134
إِذْ نَجَّيْنَـٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,. [134]
★
37 : 135
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَـٰبِرِينَ
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. [135]
★
37 : 136
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo. [136]
★
37 : 137
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,. [137]
★
37 : 138
وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?. [138]
★
37 : 139
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume. [139]
★
37 : 140
إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni. [140]
★
37 : 141
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. [141]
★
37 : 142
فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. [142]
★
37 : 143
فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,. [143]
★
37 : 144
لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa. [144]
★
37 : 145
۞ فَنَبَذْنَـٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa. [145]
★
37 : 146
وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye. [146]
★
37 : 147
وَأَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi. [147]
★
37 : 148
فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَـٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda. [148]
★
37 : 149
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?. [149]
★
37 : 150
أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِنَـٰثًا وَهُمْ شَـٰهِدُونَ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?. [150]
★
37 : 151
أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:. [151]
★
37 : 152
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَـٰذِبُونَ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!. [152]
★
37 : 153
أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?. [153]
★
37 : 154
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?. [154]
★
37 : 155
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Hamkumbuki?. [155]
★
37 : 156
أَمْ لَكُمْ سُلْطَـٰنٌ مُّبِينٌ
Au mnayo hoja iliyo wazi?. [156]
★
37 : 157
فَأْتُوا۟ بِكِتَـٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli. [157]
★
37 : 158
وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa. [158]
★
37 : 159
سُبْحَـٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. [159]
★
37 : 160
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [160]
★
37 : 161
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu. [161]
★
37 : 162
مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَـٰتِنِينَ
Hamwezi kuwapoteza. [162]
★
37 : 163
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni. [163]
★
37 : 164
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu. [164]
★
37 : 165
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. [165]
★
37 : 166
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. [166]
★
37 : 167
وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:. [167]
★
37 : 168
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,. [168]
★
37 : 169
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. [169]
★
37 : 170
فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua. [170]
★
37 : 171
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa. [171]
★
37 : 172
إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. [172]
★
37 : 173
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَـٰلِبُونَ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda. [173]
★
37 : 174
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Basi waachilie mbali kwa mda. [174]
★
37 : 175
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Na watazame, nao wataona. [175]
★
37 : 176
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?. [176]
★
37 : 177
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa. [177]
★
37 : 178
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Na waache kwa muda. [178]
★
37 : 179
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Na tazama, na wao wataona. [179]
★
37 : 180
سُبْحَـٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. [180]
★
37 : 181
وَسَلَـٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
Na Salamu juu ya Mitume. [181]
★
37 : 182
وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. [182]
★