51 : 1
وَٱلذَّٰرِيَـٰتِ ذَرْوًا
Naapa kwa pepo zinazo tawanya! [1]
★
51 : 2
فَٱلْحَـٰمِلَـٰتِ وِقْرًا
Na zinazo beba mizigo! [2]
★
51 : 3
فَٱلْجَـٰرِيَـٰتِ يُسْرًا
Na zinazo kwenda kwa wepesi. [3]
★
51 : 4
فَٱلْمُقَسِّمَـٰتِ أَمْرًا
Na zinazo gawanya kwa amri! [4]
★
51 : 5
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli! [5]
★
51 : 6
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea. [6]
★
51 : 7
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ
Naapa kwa mbingu zenye njia! [7]
★
51 : 8
إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana. [8]
★
51 : 9
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa. [9]
★
51 : 10
قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ
Wazushi wameangamizwa. [10]
★
51 : 11
ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍ سَاهُونَ
Ambao wameghafilika katika ujinga. [11]
★
51 : 12
يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo? [12]
★
51 : 13
يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni. [13]
★
51 : 14
ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza. [14]
★
51 : 15
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. [15]
★
51 : 16
ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. [16]
★
51 : 17
كَانُوا۟ قَلِيلًا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. [17]
★
51 : 18
وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira. [18]
★
51 : 19
وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba. [19]
★
51 : 20
وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَـٰتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini. [20]
★
51 : 21
وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni? [21]
★
51 : 22
وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa. [22]
★
51 : 23
فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema. [23]
★
51 : 24
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa? [24]
★
51 : 25
إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَـٰمًا ۖ قَالَ سَلَـٰمٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni. [25]
★
51 : 26
فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona. [26]
★
51 : 27
فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli? [27]
★
51 : 28
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا۟ لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَـٰمٍ عَلِيمٍ
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu. [28]
★
51 : 29
فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa! [29]
★
51 : 30
قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua. [30]
★
51 : 31
۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa? [31]
★
51 : 32
قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu, [32]
★
51 : 33
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
Tuwatupie mawe ya udongo, [33]
★
51 : 34
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka. [34]
★
51 : 35
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini. [35]
★
51 : 36
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu! [36]
★
51 : 37
وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu. [37]
★
51 : 38
وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi. [38]
★
51 : 39
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَـٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu! [39]
★
51 : 40
فَأَخَذْنَـٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَـٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa. [40]
★
51 : 41
وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi. [41]
★
51 : 42
مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka. [42]
★
51 : 43
وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍ
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu. [43]
★
51 : 44
فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona. [44]
★
51 : 45
فَمَا ٱسْتَطَـٰعُوا۟ مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea. [45]
★
51 : 46
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًا فَـٰسِقِينَ
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu. [46]
★
51 : 47
وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَـٰهَا بِأَيْي۟دٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua. [47]
★
51 : 48
وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَـٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَـٰهِدُونَ
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi! [48]
★
51 : 49
وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie. [49]
★
51 : 50
فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. [50]
★
51 : 51
وَلَا تَجْعَلُوا۟ مَعَ ٱللَّهِ إِلَـٰهًا ءَاخَرَ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake. [51]
★
51 : 52
كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا۟ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu. [52]
★
51 : 53
أَتَوَاصَوْا۟ بِهِۦ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi. [53]
★
51 : 54
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٍ
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi. [54]
★
51 : 55
وَذَكِّرْ فَإِنَّ ٱلذِّكْرَىٰ تَنفَعُ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini. [55]
★
51 : 56
وَمَا خَلَقْتُ ٱلْجِنَّ وَٱلْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi. [56]
★
51 : 57
مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti. [57]
★
51 : 58
إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلْقُوَّةِ ٱلْمَتِينُ
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti. [58]
★
51 : 59
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَـٰبِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize. [59]
★
51 : 60
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِن يَوْمِهِمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa. [60]
★