70 : 1
سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea! [1]
★
70 : 2
لِّلْكَـٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌ
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia . [2]
★
70 : 3
مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja. [3]
★
70 : 4
تَعْرُجُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu! [4]
★
70 : 5
فَٱصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا
Basi subiri kwa subira njema.Hakika wao wanaiona iko mbali! [5]
★
70 : 6
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًا
Hakika wao wanaiona iko mbali! [6]
★
70 : 7
وَنَرَىٰهُ قَرِيبًا
Na Sisi tunaiona iko karibu. [7]
★
70 : 8
يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa. [8]
★
70 : 9
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ
Na milima itakuwa kama sufi. [9]
★
70 : 10
وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake. [10]
★
70 : 11
يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe, [11]
★
70 : 12
وَصَـٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
Na mkewe, na nduguye, [12]
★
70 : 13
وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu, [13]
★
70 : 14
وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye. [14]
★
70 : 15
كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa, [15]
★
70 : 16
نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ
Unao babua ngozi ya kichwa! [16]
★
70 : 17
تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka. [17]
★
70 : 18
وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi. [18]
★
70 : 19
۞ إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
Hakika mtu ameumbwa na papara. [19]
★
70 : 20
إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًا
Inapo mgusa shari hupapatika. [20]
★
70 : 21
وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا
Na inapo mgusa kheri huizuilia. [21]
★
70 : 22
إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ
Isipo kuwa wanao swali, [22]
★
70 : 23
ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ
Ambao wanadumisha Sala zao, [23]
★
70 : 24
وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu [24]
★
70 : 25
لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba; [25]
★
70 : 26
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo, [26]
★
70 : 27
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi. [27]
★
70 : 28
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo. [28]
★
70 : 29
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَـٰفِظُونَ
Na ambao wanahifadhi tupu zao. [29]
★
70 : 30
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَـٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi [30]
★
70 : 31
فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka. [31]
★
70 : 32
وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَـٰنَـٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao, [32]
★
70 : 33
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَـٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao, [33]
★
70 : 34
وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ
Na ambao wanazihifadhi Sala zao. [34]
★
70 : 35
أُو۟لَـٰٓئِكَ فِى جَنَّـٰتٍ مُّكْرَمُونَ
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi. [35]
★
70 : 36
فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu? [36]
★
70 : 37
عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto! [37]
★
70 : 38
أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema? [38]
★
70 : 39
كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua. [39]
★
70 : 40
فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَـٰرِقِ وَٱلْمَغَـٰرِبِ إِنَّا لَقَـٰدِرُونَ
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza [40]
★
70 : 41
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi. [41]
★
70 : 42
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَـٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa, [42]
★
70 : 43
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo, [43]
★
70 : 44
خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa. [44]
★