75 : 1
لَآ أُقْسِمُ بِيَوْمِ ٱلْقِيَـٰمَةِ
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama! [1]
75 : 2
وَلَآ أُقْسِمُ بِٱلنَّفْسِ ٱللَّوَّامَةِ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu! [2]
75 : 3
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَـٰنُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُۥ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake? [3]
75 : 4
بَلَىٰ قَـٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّىَ بَنَانَهُۥ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! [4]
75 : 5
بَلْ يُرِيدُ ٱلْإِنسَـٰنُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُۥ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake. [5]
75 : 6
يَسْـَٔلُ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلْقِيَـٰمَةِ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? [6]
75 : 7
فَإِذَا بَرِقَ ٱلْبَصَرُ
Basi jicho litapo dawaa! [7]
75 : 8
وَخَسَفَ ٱلْقَمَرُ
Na mwezi utapo patwa! [8]
75 : 9
وَجُمِعَ ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ
Na likakusanywa jua na mwezi! [9]
75 : 10
يَقُولُ ٱلْإِنسَـٰنُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ ٱلْمَفَرُّ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio? [10]
75 : 11
كَلَّا لَا وَزَرَ
La! Hapana pa kukimbilia! [11]
75 : 12
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمُسْتَقَرُّ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu. [12]
75 : 13
يُنَبَّؤُا۟ ٱلْإِنسَـٰنُ يَوْمَئِذٍۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha. [13]
75 : 14
بَلِ ٱلْإِنسَـٰنُ عَلَىٰ نَفْسِهِۦ بَصِيرَةٌ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake. [14]
75 : 15
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru. [15]
75 : 16
لَا تُحَرِّكْ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِۦٓ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka. [16]
75 : 17
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُۥ وَقُرْءَانَهُۥ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha. [17]
75 : 18
فَإِذَا قَرَأْنَـٰهُ فَٱتَّبِعْ قُرْءَانَهُۥ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake. [18]
75 : 19
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُۥ
Kisha ni juu yetu kuubainisha. [19]
75 : 20
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani, [20]
75 : 21
وَتَذَرُونَ ٱلْـَٔاخِرَةَ
Na mnaacha maisha ya Akhera. [21]
75 : 22
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara, [22]
75 : 23
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi. [23]
75 : 24
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍۭ بَاسِرَةٌ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana. [24]
75 : 25
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo. [25]
75 : 26
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِىَ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo, [26]
75 : 27
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga? [27]
75 : 28
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلْفِرَاقُ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki; [28]
75 : 29
وَٱلْتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi, [29]
75 : 30
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ ٱلْمَسَاقُ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi! [30]
75 : 31
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakuswali. [31]
75 : 32
وَلَـٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Bali alikanusha, na akageuka. [32]
75 : 33
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao. [33]
75 : 34
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
Ole wako, ole wako! [34]
75 : 35
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰٓ
Kisha Ole wako, ole wako! [35]
75 : 36
أَيَحْسَبُ ٱلْإِنسَـٰنُ أَن يُتْرَكَ سُدًى
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure? [36]
75 : 37
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِىٍّ يُمْنَىٰ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa? [37]
75 : 38
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo. [38]
75 : 39
فَجَعَلَ مِنْهُ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke. [39]
75 : 40
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَـٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحْـِۧىَ ٱلْمَوْتَىٰ
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu? [40]