77 : 1
وَٱلْمُرْسَلَـٰتِ عُرْفًا
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole! [1]
★
77 : 2
فَٱلْعَـٰصِفَـٰتِ عَصْفًا
Na zinazo vuma kwa kasi! [2]
★
77 : 3
وَٱلنَّـٰشِرَٰتِ نَشْرًا
Na zikaeneza maeneo yote! [3]
★
77 : 4
فَٱلْفَـٰرِقَـٰتِ فَرْقًا
Na zinazo farikisha zikatawanya! [4]
★
77 : 5
فَٱلْمُلْقِيَـٰتِ ذِكْرًا
Na zinazo peleka mawaidha! [5]
★
77 : 6
عُذْرًا أَوْ نُذْرًا
Kwa kuudhuru au kuonya, [6]
★
77 : 7
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٌ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa! [7]
★
77 : 8
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتْ
Wakati nyota zitakapo futwa, [8]
★
77 : 9
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتْ
Na mbingu zitakapo pasuliwa, [9]
★
77 : 10
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ نُسِفَتْ
Na milima itakapo peperushwa, [10]
★
77 : 11
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتْ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao, [11]
★
77 : 12
لِأَىِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo? [12]
★
77 : 13
لِيَوْمِ ٱلْفَصْلِ
Kwa siku ya kupambanua! [13]
★
77 : 14
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini? [14]
★
77 : 15
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha! [15]
★
77 : 16
أَلَمْ نُهْلِكِ ٱلْأَوَّلِينَ
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia? [16]
★
77 : 17
ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ ٱلْـَٔاخِرِينَ
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia? [17]
★
77 : 18
كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu! [18]
★
77 : 19
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [19]
★
77 : 20
أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّآءٍ مَّهِينٍ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa? [20]
★
77 : 21
فَجَعَلْنَـٰهُ فِى قَرَارٍ مَّكِينٍ
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti? [21]
★
77 : 22
إِلَىٰ قَدَرٍ مَّعْلُومٍ
Mpaka muda maalumu? [22]
★
77 : 23
فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ ٱلْقَـٰدِرُونَ
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria. [23]
★
77 : 24
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [24]
★
77 : 25
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ كِفَاتًا
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya [25]
★
77 : 26
أَحْيَآءً وَأَمْوَٰتًا
Walio hai na maiti? [26]
★
77 : 27
وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ شَـٰمِخَـٰتٍ وَأَسْقَيْنَـٰكُم مَّآءً فُرَاتًا
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu? [27]
★
77 : 28
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [28]
★
77 : 29
ٱنطَلِقُوٓا۟ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha! [29]
★
77 : 30
ٱنطَلِقُوٓا۟ إِلَىٰ ظِلٍّ ذِى ثَلَـٰثِ شُعَبٍ
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu! [30]
★
77 : 31
لَّا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِى مِنَ ٱللَّهَبِ
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako. [31]
★
77 : 32
إِنَّهَا تَرْمِى بِشَرَرٍ كَٱلْقَصْرِ
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba! [32]
★
77 : 33
كَأَنَّهُۥ جِمَـٰلَتٌ صُفْرٌ
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano! [33]
★
77 : 34
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [34]
★
77 : 35
هَـٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu, [35]
★
77 : 36
وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru. [36]
★
77 : 37
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha! [37]
★
77 : 38
هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَـٰكُمْ وَٱلْأَوَّلِينَ
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia. [38]
★
77 : 39
فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ
kiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi! [39]
★
77 : 40
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha! [40]
★
77 : 41
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى ظِلَـٰلٍ وَعُيُونٍ
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem, [41]
★
77 : 42
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ
Na matunda wanayo yapenda, [42]
★
77 : 43
كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda. [43]
★
77 : 44
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema. [44]
★
77 : 45
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [45]
★
77 : 46
كُلُوا۟ وَتَمَتَّعُوا۟ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu! [46]
★
77 : 47
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [47]
★
77 : 48
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرْكَعُوا۟ لَا يَرْكَعُونَ
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami. [48]
★
77 : 49
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! [49]
★
77 : 50
فَبِأَىِّ حَدِيثٍۭ بَعْدَهُۥ يُؤْمِنُونَ
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini? [50]
★