78 : 1
عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
WANAULIZANA nini? [1]
★
78 : 2
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ
Ile khabari kuu! [2]
★
78 : 3
ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana. [3]
★
78 : 4
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
La! Karibu watakuja jua. [4]
★
78 : 5
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Tena la! Karibu watakuja jua. [5]
★
78 : 6
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَـٰدًا
kaKwani hatukuifanya ardhi ma tandiko? [6]
★
78 : 7
وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًا
kama Na milima vigingi? [7]
★
78 : 8
وَخَلَقْنَـٰكُمْ أَزْوَٰجًا
Na tukakuumbeni kwa jozi? [8]
★
78 : 9
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko? [9]
★
78 : 10
وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًا
Na tukaufanya usiku ni nguo? [10]
★
78 : 11
وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًا
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha? [11]
★
78 : 12
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu? [12]
★
78 : 13
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto; [13]
★
78 : 14
وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءً ثَجَّاجًا
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni, [14]
★
78 : 15
لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّا وَنَبَاتًا
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea. [15]
★
78 : 16
وَجَنَّـٰتٍ أَلْفَافًا
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana. [16]
★
78 : 17
إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَـٰتًا
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake, [17]
★
78 : 18
يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi, [18]
★
78 : 19
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًا
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango. [19]
★
78 : 20
وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi. [20]
★
78 : 21
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا
Hakika Jahannamu inangojea! [21]
★
78 : 22
لِّلطَّـٰغِينَ مَـَٔابًا
Kwa walio asi ndio makaazi yao, [22]
★
78 : 23
لَّـٰبِثِينَ فِيهَآ أَحْقَابًا
Wakae humo karne baada ya karne, [23]
★
78 : 24
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji, [24]
★
78 : 25
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا
Ila maji yamoto sana na usaha, [25]
★
78 : 26
جَزَآءً وِفَاقًا
Ndio jaza muwafaka. [26]
★
78 : 27
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ حِسَابًا
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu. [27]
★
78 : 28
وَكَذَّبُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا كِذَّابًا
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu. [28]
★
78 : 29
وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَـٰهُ كِتَـٰبًا
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika. [29]
★
78 : 30
فَذُوقُوا۟ فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu! [30]
★
78 : 31
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu, [31]
★
78 : 32
حَدَآئِقَ وَأَعْنَـٰبًا
Mabustani na mizabibu, [32]
★
78 : 33
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا
Na wake walio lingana nao, [33]
★
78 : 34
وَكَأْسًا دِهَاقًا
Na bilauri zilizo jaa, [34]
★
78 : 35
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّٰبًا
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo, [35]
★
78 : 36
جَزَآءً مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابًا
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha. [36]
★
78 : 37
رَّبِّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ٱلرَّحْمَـٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake! [37]
★
78 : 38
يَوْمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَـٰنُ وَقَالَ صَوَابًا
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu. [38]
★
78 : 39
ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلْحَقُّ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi [39]
★
78 : 40
إِنَّآ أَنذَرْنَـٰكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ ٱلْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلْكَافِرُ يَـٰلَيْتَنِى كُنتُ تُرَٰبًۢا
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo! [40]
★