88 : 1
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَـٰشِيَةِ
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza? [1]
★
88 : 2
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَـٰشِعَةٌ
Siku hiyo nyuso zitainama! [2]
★
88 : 3
عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ
Zikifanya kazi, nazo taabani. [3]
★
88 : 4
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً
Ziingie katika Moto unao waka . [4]
★
88 : 5
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka. [5]
★
88 : 6
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba. [6]
★
88 : 7
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa. [7]
★
88 : 8
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu. [8]
★
88 : 9
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao! [9]
★
88 : 10
فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
Katika Bustani ya juu. [10]
★
88 : 11
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَـٰغِيَةً
Hawatasikia humo upuuzi.Humo imo chemchem inayo miminika. [11]
★
88 : 12
فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ
Humo imo chemchem inayo miminika. [12]
★
88 : 13
فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa, [13]
★
88 : 14
وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ
Na bilauri zilizo pangwa, [14]
★
88 : 15
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ
Na matakia safu safu, [15]
★
88 : 16
وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ
Na mazulia yaliyo tandikwa. [16]
★
88 : 17
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa? [17]
★
88 : 18
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa? [18]
★
88 : 19
وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa? [19]
★
88 : 20
وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa? [20]
★
88 : 21
فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. [21]
★
88 : 22
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
Wewe si mwenye kuwatawalia. [22]
★
88 : 23
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa, [23]
★
88 : 24
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa! [24]
★
88 : 25
إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao. [25]
★
88 : 26
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao! [26]
★