90 : 1
لَآ أُقْسِمُ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu! [1]
90 : 2
وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu. [2]
90 : 3
وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa. [3]
90 : 4
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ فِى كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu. [4]
90 : 5
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza? [5]
90 : 6
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali. [6]
90 : 7
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona? [7]
90 : 8
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ
Kwani hatukumpa macho mawili? [8]
90 : 9
وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ
Na ulimi, na midomo miwili? [9]
90 : 10
وَهَدَيْنَـٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ
Na tukambainishia zote njia mbili? [10]
90 : 11
فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. [11]
90 : 12
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? [12]
90 : 13
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa; [13]
90 : 14
أَوْ إِطْعَـٰمٌ فِى يَوْمٍ ذِى مَسْغَبَةٍ
Au kumlisha siku ya njaa [14]
90 : 15
يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa, [15]
90 : 16
أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ
Au masikini aliye vumbini. [16]
90 : 17
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. [17]
90 : 18
أُو۟لَـٰٓئِكَ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani. [18]
90 : 19
وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا هُمْ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni. [19]
90 : 20
عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande. [20]