96 : 1
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba! [1]
★
96 : 2
خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ مِنْ عَلَقٍ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu! [2]
★
96 : 3
ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote! [3]
★
96 : 4
ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ
Ambaye amefundisha kwa kalamu. [4]
★
96 : 5
عَلَّمَ ٱلْإِنسَـٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui. [5]
★
96 : 6
كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ لَيَطْغَىٰٓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri. [6]
★
96 : 7
أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ
Akijiona katajirika. [7]
★
96 : 8
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo. [8]
★
96 : 9
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
Umemwona yule anaye mkataza. [9]
★
96 : 10
عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Mja anapo sali? [10]
★
96 : 11
أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu? [11]
★
96 : 12
أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ
Au anaamrisha uchamngu? [12]
★
96 : 13
أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma? [13]
★
96 : 14
أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona? [14]
★
96 : 15
كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele! [15]
★
96 : 16
نَاصِيَةٍ كَـٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍ
Shungi la uwongo, lenye makosa! [16]
★
96 : 17
فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awaite wenzake! [17]
★
96 : 18
سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Nasi tutawaita Mazabania! [18]
★
96 : 19
كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee! [19]
★