99 : 1
إِذَا زُلْزِلَتِ ٱلْأَرْضُ زِلْزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! [1]
★
99 : 2
وَأَخْرَجَتِ ٱلْأَرْضُ أَثْقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake! [2]
★
99 : 3
وَقَالَ ٱلْإِنسَـٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini? [3]
★
99 : 4
يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake. [4]
★
99 : 5
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia! [5]
★
99 : 6
يَوْمَئِذٍ يَصْدُرُ ٱلنَّاسُ أَشْتَاتًا لِّيُرَوْا۟ أَعْمَـٰلَهُمْ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! [6]
★
99 : 7
فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! [7]
★
99 : 8
وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! [8]
★